Wednesday, July 6, 2011

Chuo cha KAM kinavyojizatiti kuzalisha wataalam ktk sekta ya afya

Chuo cha Afya cha KAM kilichopo Kimara Mavurunza, jijini Dar es Salaam ambacho sasa kimesajiliwa na NACTE kwa kumbukumbu Na NACTE/BA/436/605/vol.xvi/98, kinatarajiwa kupata wanafunzi 30 ifikapo Septemba mwaka huu.
Mwenyekiti wa chuo hicho, Dk. Kandole Musika alisema kuwa kwa sasa kina wanafunzi 80 na kwamba kufikia wakati huo wa mwezi Septemba idadi ya wanafunzi wanaohitajika itakuwa imetimia.
"Chuo kinatarajia kuchukuwa wanafunzi 300, lakini kwa sasa wameanza 80 wakati taratibu nyingine zikiendelea hadi kufikia Septemba ambapo wataongezeka wengine zaidi," alisema.
Alisema kuwa masomo yanayotolewa chuoni hapo kwa sasa fani za wataalam wa Maabara yaani Medical Laboratory na Utabibu (Clinical Medicine).
"Baada ya chuo kutoa fani hizo kwa muda, baadaye kitaanza kujikita pia katika ufundishaji wa taaluma ya uuzaji na utoaji dawa (famasia) na wataalam wauguzi (Nursey)," alisema.
Aliongeza kusema kuwa ni imani yake kwamba baada ya miaka miwili kitaanza kutoa mchango kwa serikali kwa kupunguza tatizo la uhaba wa wataalam wa afya katika fani za maabara na utabibu.
Aidha, alisema KAM imefanikiwa kujenga madarasa nane, maabara kwa ajili ya mazoezi kwa vitendo chuoni hapo  pamoja na mabweni 15 yenye uwezo wa kulaza wanafunzi nane kila moja.
"KAM College of Health Sciences ambacho kilianza kupokea wanafunzi Machi mwaka huu, kimethibitishwa rasmi Mei 19' 2011 kina uhakika wa kutoa wataalam wa afya miaka michache ijayo," alisema.

1 comment:

  1. hongera sana Dr.Kandole Musika kwa juhudi zako za kuzalisha wataalamu wa afya nchini mwetu,Mungu abariki kazi ya mikono yako

    ReplyDelete