Thursday, July 21, 2011

Chuo kipya cha Ualimu chaanzishwa Mbezi Kwa Yusuph, Dar es Salaam.

Chuo kipya cha Ualimu kimeanzishwa Mbezi Kwa Yusuph, jijini Dar es Salaam kinachojulikana kama Mbezi Teacher's Training College ambacho kinatarajia kuanza kupokea wanafunzi Julai 25 kwa ajili ya masomo.
Tayari baadhi ya wanafunzi wameshaanza kujisajili kwa ajili ya masomo yao chuoni hapo huku Mkuu wa chuo hicho, David Msuya akisema kuwa chuo hicho kina mandhari nzuri ya kuwavutia wanafunzi.
Mbali na hilo, mkuu huyo wa chuo anasema kuwa kimesheheni kila kitu kuanzia maktaba, maabara, mabweni  na vitu vingine vinavyotakiwa katika vyuo vya ualimu hapa nchini.
"Pia tuna walimu wa kutosha wenye ujuzi na uzoefu wa kutosha kwenye kazi ya ufundishaji, hivyo nina uhakika wanafunzi watakaokuja kusoma hapa wataridhika na kile watakachokipata.

No comments:

Post a Comment