Wednesday, July 6, 2011

Mbunge Jimbo la Ruangwa mkoani Lindi, Kassim Majaliwa aendelea kuwasaidia wananchi wa jimbo lake.

Baadhi ya wakazi wa kata ya Chinongwe jimbo la Ruangwa mkoani Lindi ambao hivi karibuni walioathiriwa na mvua, wamepata msaada wa unga na mabati ili visaidie kuendesha maisha yao ya kila siku
Msaada huo ulitolewa na mbunge wa jimbo hilo ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) anayeshughulikia elimu, Kassim Majaliwa.
Kila mara mbunge huyo amekuwa akifika jimboni mwake humo kuwajulia hali wapiga kura wake na kuwatatulia kero mbalimbali zinazowakabili kulingana na hali inavyoruhusu.
Jimbo la Ruangwa lina kata 21 ambapo mbunge huyo ameshatembelea kata zaidi ya 10 kwa ajili ya kuwashukuru wapiga kura wake na pia kutatua baadhi ya kero zinazowakabili.
Yeye binafsi anasema, kuwa karibu na wananchi ndio njia pekee ya kujua matatizo na changamoto zinazowakabili na pia njia mojawapo ambayo itasaidia kubuni na kuibua mkakati wa kuwaletea maendeleo.
"Nitaendelea kuwatembelea wapiga kura wangu kwa sababu nimeahidi kuwatumikia kwa nafasi hii ya ubunge, hivyo ninawajibika kuwatembelea na kuwajulia hali na hata kusaidina nao kutatua kero mbalimbali
zinazowakabili," alisema Majaliwa.

No comments:

Post a Comment