Wednesday, July 6, 2011

Mbunge wa Jimbo la Musoma Mjini atembelea wagonjwa hospitalini

Moja ya majukumbu ya mbunge ni kutembelea wananchi wake wakati wa shida na hata wa raha kama ambavyo amekuwa akifanya mbunge wa Jimbo la Musoma Mjini, mkoani Mara, Vicent Nyerere awapo jimboni mwake ambapo pamoja na kusimamia miradi mbalimbali ya maendeleo kwa ajili ya jimbo hilo, amekuwa akitembea kwenye hospitali ili kuwajulia hali wagonjwa.
Yeye mwenyewe anasema kuwa siyo hospitali tu bali hutembelea pia kwenye magereza ili kuwajulia hali wafungwa na mahabusu na kuwasaidia kwa chochote pale inapowezekana, kwa kuwa wao pia ni binadamu wana matatizo yanaowakabili huko magerezani.

No comments:

Post a Comment