Wednesday, July 6, 2011

Sera ya Ukimwi Mahali pa kazi yafanya watumishi wengi kuwa wazi

Sera ya Ukimwi Mahali ya pa Kazi imechangia watumishi wengi kuwa wazi mara wanapotambua kuwa wameathirika kwa ugonjwa huo hatari na hivyo kuwafanya wafuate maelekezo ya jinsi ya kuishi kwa matumain kwa kutumia dawa za kurefusha maisha.
Hayo yaliwekwa wazi hivi karibuni kwenye semina iliyowashirikisha askari polisi, waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari ikiratibiwa na viongozi wa Chama cha Waandishi wa Habari za Ukimwi nchini AJAAT.
Semina hiyo iliendeshwa na Mkuu wa Mawasiliano wa Marie Stopes, Johnbosco Baso kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya na kufanyika ukumbi wa Wanyama Hotel, Sinza jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment